Text

Amua Kuongozwa na Uwepo wa Mungu

1 views 1 day ago

KUTOKA 33:14-15 

“Akasema, Uso wangu utakwenda pamoja nawe, nami nitakupa raha. Naye akamwambia, Uso wako usipokwenda pamoja nami, usituchukue kutoka hapa.”

EXODUS 33:14-15 AMP

“And the LORD said, “My presence shall go with you, and I will give you rest [by bringing you and the people into the promised land].” And Moses said to Him, “If Your presence does not go [with me], do not lead us up from here.”

Mungu alimwambia Musa kuwa, "Akasema, Uso wangu utakwenda pamoja nawe, nami nitakupa raha."

Biblia ya kingereza inasema "UWEPO WANGU UTAENDA NAWE, nami nitakupa raha au pumziko"

Tafsiri ya USO WA MUNGU katika andiko hilo ni uwepo wa Mungu! 

Anaposema uso wangu utakwenda nawe maana yake ni uwepo wa Mungu utakwenda nawe!

Hilo Neno "raha" au "rest" lina maana pumziko, au faraja, au utulivu pia unaweza kuita amani!

Kwa hiyo, raha moyoni au hali ya kuwa na ushwari moyoni ni matokeo ya uwepo wa Mungu kuwa nawe na sio matokeo ya vitu vya nje!

Kuna watu wana kila kitu lakini hawana pumziko la mioyo wao, wako restless!

Kwa hiyo, UWEPO WA MUNGU UNAPOKUWA NAWE UTAKUWA NA RAHA AU AMANI AU UTULIVU NAFSINI MWAKO!

TUANGALIE KWA MTAZAMO MWINGINE:

Neno linaposema "Akasema, Uso wangu utakwenda pamoja nawe, nami nitakupa raha." Maana yake ni kwamba "Uso wangu usipokwenda nawe hutapata raha nafsini mwako(yaani utapata mahangaiko, au masumbufu au kukosa amani yaani hali ya kuwa restless)

Ukiunganisha na mstari wa 15 utaona inasema, kama uwepo wako hauendi nasi basi usituchukue kutoka hapa au usituongoze kutoka hapa!

Maana yake ni kwamba, UWEPO WA MUNGU UNAWEZA KUMUONGOZA MTU KUTOKA SEHEMU MOJA KWENDA NYINGINE ALIYOIKUSUDIA MUNGU, au pia UNAWEZA KUMZUIA MTU ASIENDE MAHALI AMBAPO MUNGU HAJAPAKUSUDIA KUMPELEKA!

UWEPO WA MUNGU UNATUONGOZAJE?

- Umewahi kuwa na raha au utulivu moyoni na ghafla unapowaza kwenda sehemu fulani ule utulivu unakata?  Inawezekana kabisa uwepo wa Mungu unakuongoza kwamba usiende kule

- Umewahi kuwa uko na mtu mna maongezi na ghafla mkianza tu kuongelea jambo      fulani unasikia utulivu ndani yako unaanza kupungua na kwa kadiri unavyoendelea kuongelea jambo hilo shida inaongezeka? Inawezekana kabisa uwepo wa Mungu unakuzuia kuendelea kuongelea jambo hilo

- Umewahi kuanza uhusiano na mtu na ghafla unasikia utulivu moyoni unakata na kuondoka? Maana yake uwepo wa Mungu unakuongoza usiendelee n     a uhusiano huo au unakuambia mnahusiana kwa njia ambayo sio sahihi!

- Umewahi kuletewa mkataba kusaini ambao ukiusoma huoni kasoro yoyote lakini kila uki     fikiria kusaini unasikia unakosa raha? Basi ujue uwepo wa Mungu unakuongoza kwamba kuna kitu hakiko sawa hata kama hujakiona.

Usikubali kuondoka na kuuacha uwepo wa Mungu! 

RUHUSU UWEPO WA MUNGU UKU     SAIDIE KWENDA MAHALI SAHIHI!

“Na amani ya Kristo iamue mioyoni mwenu; ndiyo mliyoitiwa katika mwili mmoja; tena iweni watu wa shukrani.”

KOL. 3:15

Usikubali kufanya maamuzi wakati AMANI YA KRISTO UMEIACHA MAHALI!

RUHUSU UWEPO WA MUNGU UKUSAIDIE KUFANYA MAAMUZI SAHIHI!

#UponyajiWaKiMunguKwaWoteWenyeMwili
Umebarikiwa
~Na. Mwl. Francis M. Langula

 

Comments (0)
Login to leave a comment.

No comments yet. Be the first to comment!